Habari za asubuhi! Umeamshwaje! Na ndugu hapo wanaendeleaje? Mithali 24:3-4 [3]Nyumba hujengwa kwa hekima, Na kwa ufahamu huthibitika, [4]Na kwarifa vyumba vyake hujazwa Vitu vyote vya thamani na vya kupendeza. Roho wa Mungu akuangazie na kukupatia hekima kuyajenga yale yote yaliowekwa mikononi na moyoni mwako, ufahamu wake ulioko ndani yako ukathibitike na kwa maarifa yake akujaze na kuongeza thamani katika yote. Umebarikiwa. Shalom.
by RAPHAEL KIMARO.